Page:Swahili tales.djvu/92

From Wikisource
Jump to navigation Jump to search
This page has been proofread.
72
SULTANI DARAI.

mwanamke; bassi amekuletea hii, nawe mwie rathi, mstahimilie, amekuletea kitu kisichokuwa sawa nawe, kwa nini kitu kidogo.

Sultani akamwambia, Allahu, mimi ni rathi sana, mimi ni rathi sana, hatta kaburi yangu nikifa i rathi kwa haya alionitendea Sultani Darai. Akamwambia, marahaba, ahsánte, ni rathi sana, mke mkewe, ndugu nduguye, mtumwa mtumwa wake, atakapo wakati wo wote, Sultani Darai nimwoze mwanangu, sitaki pishi kwake, sitaki kisaga kwake, sitaki kibaba kwake; sitaki nussu ya kibaba kwake, sitaki robo kibaba kwake, walakini aje yee mtupu, baada ya hizi asizidi kitu tena, haya alioniletea si haba, yaliobaki na yache kuko huko, bassi ndiyo maneno yangu, ukamweleza Sultani Darai.

Bassi paa akaondoka, akamwambia, Bwana, kua heri! nami niwie rathi sana mtumwa wako. Akamwambia, mimi nimetangulia kupokea rathi zako, nami nataka uniwie rathi sana, wewe paa, kwa haya naliokujibu. Akamwambia, rathi, bwana, hatta kwa mangine, nami, bwana, ni rathi, nami, bwana, ninakwenda zangu hatta mjini kwetu, hatutakaa siku nyingi, labuda siku nane, ao siku edashara, tutakuwa tutawasili wageni wenu. Akamwambia, Ah! kua heri.

Na yule bwana wake paa katika ule mji watu wanamzomea, na watu wanamcheka, na baathi ya watu wanamguna, na baathi ya watu wangine wanamsema, amba huyu maskini ana wazimu zayidi sasa, alikuwa na themuni yake, akaenda akanunua paa, na yule paa akamwachia, sasa anazunguka na mji, na kilio, maskini paa wangu ee, maskini paa wangu. Na watu nukumcheka, naye akili zake zimepotea kwa sababu ya paa yule.