Page:Swahili tales.djvu/82

From Wikisource
Jump to navigation Jump to search
This page has been proofread.
62
SULTANI DARAI.

amini kama mimi nitaregea, nami Bwana, kua heri, nakuaga, natoka naenda zangu.

Akamwambia, haya enenda. Paa akitoka mbio, na yule maskini akatoka mbio ndani, akasimama uwanjani. Na paa amezidi kwenda mbio. Yule maskini akapigwa na msangao na machozi yakamtoka. Akapiga ukelele moja, yule maskini. Mama yangu, ee, na mikono katika kitwani. Akapiga ukelele wa pili, Baba yangu, ee! Akapiga ukelele wa tatu. Ee, paa wangu amekimbia.

Wale jirani waliopo wakaja wakamzomea, wakamwambia, wewe mpumbafu, wewe barthuli, wewe asharati, umekaa jaani siku kathawakatha, umepekua kama kuku, hatta Muungu amekupa themuni ile, usiweze kununua muhogo, ukale, ukanunua paa, tena umemwachia, walia na nini sasa, kilio cha mwenda nguu.

Akanyamaa, shukuru. Akaondoka, akaenda zake maskini, akaenda pale jaani pake, akapata punje za mtama, akarudi nyumbani, akafanya ukiwa.

Hatta yalipokoma maghrebi akija paa wake. Akacheka sana maskini, Muungu akusimika, ah! umekuja baba.

Akamwambia, si ule wahadi naliokupa? Akamwambia, nakuona themuni walionunua mimi kwako, ndio lakki yako ya mali, nami naona hasara utwae lakki yako ya mali enda kuwapa watu wangine sasa nikikukimbia. Nimekwenda zangu mwituni, amekwenda mtu ameninasa ao methali amekuja mtu amenipiga bunduki; amenipata mtu mgine. Bassi uthia wote unipatao wa nini nikutie hasarani, siwezi. Nikikwenda nikichuma, jioni nije nilale.