Page:Swahili tales.djvu/72

From Wikisource
Jump to navigation Jump to search
This page has been proofread.
52
SULTANI DARAI.

alichokipata siku ile, ile themuni ya mzinga, na maji ya kunywa, na tumbako kutafuna. Akapanda kitandani kulala.

Hatta ussubui walipokucha, akaenda zake jaani. Akitupa macho njia kuu, amwona muhadimu na tundu la mibaazi. Akamwita, Ee! Muhadimu, umechukua nini ndani ya tundu hilo? Akamwambia, Paa! Paa! Akamwambia, Lete! Lete!

Pana watu wamesimama watatu, wakamwambia, wewe muhadimu, una kazi. Kwa nini, bwana zangu? Yule masikini hana cho chote, hohe hahe. Akawaambia, labuda bwana anayo. Hanayo, wamwona nawe jaani haondoki, hupekua kama kuku, killa siku hupata punje mbili za mtama, akatafuna; kama ana kitu, hangalinunua mtama akale, angetaka kununua paa? Hawezi kujilisha nafsi yake, ataweza kumlisha paa?

Akawaambia muhadimu, Yee, bwana, simjui mimi, nimechukua biashara, aniitaye yote namwitika, na akiniambia njoo, nikaenda, nitamjua huyu mnunuzi ao huyu si mnunuzi? Ntagomba na watu? nimechukua biashara nikiitwa nisiende? Ada ya mchukua biashara, aitwaye na yo yote hwenenda, akiwa mdogo akiwa mkubwa, akiwa mke, akiwa maskini, akiwa fukara, mimi hayo siyajui, mimi mchukua biashara, aniitaye yote huenenda.

Oo, bassi wewe husikii maneno yetu hayo tuliokwambia, tumeona kwake, nasi twamjua kama huyu si mnunuzi. Akaondoka yule wa pili akamwambia, Hoo! maneno gani hayo, labuda Muungu amempa, ao Muungu atakapompa, atakwambia leo fullani nimempa, njoo mtezame?