Page:Swahili tales.djvu/460

From Wikisource
Jump to navigation Jump to search
This page has been proofread.

HADITHI YA LIONGO.


Hapo zamani za Shanga palikuwa mtu, jina lake Liongo, naye ana nguvu saaa, mtu mkubwa sana katika mji. Akauthi mno watu, hatta siku hiyo, wakafanya shauri kumwendea nyumbani kwake kumfunga. Wakaenda watu wengi sana wakamingilia nyumbani gháfula, wakamkamata wakamfunga, wakaenda naye hatta gerezani, wakamtia.

Akakaa siku nyingi, akafanya hila hatta kufungua. Akatoka nje, akauthi watu vilevile, siku nyingi. Watu hawawezi kwenda mashamba, wala kukata kuni, wala kuteka maji. Wakauthika sana.

Watu wakasema, tufanye hila gani, hatta tumpate, tumwue? Akanena mmoja, tumwendee anapolala, tuniwulie mbali. Wakasema wangine, mkimpata, mfungeni, mmlete. Wakaenda wakafanya hila, hatta wakampata, wakamfunga, wakamchukua mjini. Wakaenda wakamfunga mnyororo, na pingu, na mti kati.

Wakamwacha siku nyingi, mamaye humpelekea kula kulla siku. Na mbele ya mlango kule alikofungwa, wamewekwa asikari wanayomngojea, hawaondoki marra moja ela kwa zamu.

Siku nyingi na miezi mingi imepita. Kulla siku,