Page:Swahili tales.djvu/456

From Wikisource
Jump to navigation Jump to search
This page has been proofread.

SIMBA NA KULUNGU.


Hapo kale palikuwa na simba, akachukua mimba, akavyaa mtoto. Alipokwisha vyaa mtoto, akashikwa ni njaa siku saba. Akasema, nitatoka kwa nje nitafute chakula. Alipotoka nje akamwona kulungu alisha. Akamnyatia. Yule kulungu akazungusha shingo, akamwona simba, akamwambia, Hachi, mjomba! Huyu simba akafanya haya, saipate kunikamata; amemgeua kumfanyiza mjumbawe.