Page:Swahili tales.djvu/450

From Wikisource
Jump to navigation Jump to search
This page has been proofread.
430
NYANI, NA SIMBA, NA NYOKA.

kana waweza kufanya dawa, twataka ukafanye dawa. Akasema, mimi sijui kufanya dawa.

Hatta akafika njiani, aona ndoo, pana kisima kando. Asema, nende 'kanywe maji pale kisimani. Akafika kisimani, akaona pandepande ya ndoo. Akasema, nichungulie hiki kisima cha maji, nipate maji ninywe. Hatima akachungulia mle kisimani amwona nyoka mkubwa. Akamwambia, bin Adamu, nisaburi kwanza. Yule nyoka akatoka kisimani, akamwambia, bin Adamu, wenda api? Umenifahamu? Akasema, sikujui. Akamwambia, ni mimi uliyenitoa katika mtego wako, hakuambia, nitoa wa mvua, nami nije nikutoe wa jua, nawe mgeni wendako, illakini lete huwo mkoba wako nikutilie vitu vyende vyakufale nawe huko wendako. Akampa ule mkoba, akamtilia mikufu ya thahabu, na mikufu ya fetha. Akamwambia, chukua ukatumie mkoba tele.

Alipofika katika mji, ule mji aliokwenda, alipofika awali akakutana na mtu yule, aliyeguiwa ni mtego. Akampokea mkoba, akaenda nao hatta nyumbani kwakwe. Alipomwona yule mgeni mkewe, akapika uji, akasema, nampikia mgeni wetu.

Yule mwanamume aliyemtoa katika mtego akaenda hatta kwa Sultani mle katika mji, akamwambia Sultani, yule mgeni anayekuja kule kwangu, msithani kwamba bin Adamu, ndiye nyoka, akaaye kisimani, mkathani kuwa nyoka, wala si nyoka, ni yee huyule ndiye ajigeuaye nyoka. Bassi Sultani, aenende mtu akamtwae na mkoba wakwe, nimeona na mikufu ya thahabu, na mikufu ya fetha.