Page:Swahili tales.djvu/444

From Wikisource
Jump to navigation Jump to search
This page has been proofread.

NYANI, NA SIMBA, NA NYOKA.


Hapo kale palikuwa na mji, pana mwanamke, akachukua mimba, mumewe akafa. Alipokufa mume akakaa hatima kuzaa mtoto mume. Na yule mume amali yake kutega mitego, akaguia nyama, akauza vyakula.

Hatima kufa kwake yule mwanamke akauzwa ni mtoto wakwe, mama twafa na njaa. Akamwambia yule mwana, akamwuza mamaye, mama, baba alikuwa kufanya kazi gani, akavumbua chakula? Akamwambia, babayo kevu akatega mitego akavumbua chakula. Bassi nami 'tatega mitego, nipate nyama, tupate uza, tupate chakula.

Akasinda kutwa, akakata matawi ya miti. Siku ya pili, akasinda kutwa, akakata mitego. Siku ya tatu akasinda kutwa, akapakasa ngole. Siku ya nne, akasinda kutwa, akasimika mitego. Siku ya tano, akasinda kutwa kutega mitego. Siku ya sita akaenda kuonja mitego, akanamua nyama, akawachinja, akapeleka nyama mjini, zikaenenda zikauzwa nafaka. Majumba yao yakajaa tele vyakula, wakapata nafasi ya ulimwengu.

Hatima akaenda akaonja mitego, haipati kitu. Siku ya