Page:Swahili tales.djvu/432

From Wikisource
Jump to navigation Jump to search
This page has been proofread.

MTU AYARI NA HAMALI.


Mtu alikuwa ayari, huenda sokoni akinunua vitu, akiisha nunua wale watwekao hawapi ujira wao.

Siku moja akanunua sanduku ya bilauri, akatafuta mtu wa kumchukulia, akapata hamali akamwambia, katika mambo mawili khitari mojawapo, kukupa ujira wako, ao nitakupa maneno matatu ya kukufaa ulimwenguni. Akamwambia, mapesa napata killa siku, nitakuchukulia kwa haya maneno matatu, utakayoniambia.

Akachukua sanduku. Akipata thulúth ya njia akamwambia, bwana wangu, sanduku hili zito, limenilemea, nipe neno moja, nipate kupata afia za kuenenda.

Akamwambia, mtu akikwambia, utumwa bora kuliko ungwana, usimsadiki.

Akamwangalia sana, akamjua, huyu mwenyi sanduku hii ni ayari, lakini ni kheri nisubiri hatta nifike. Wakaenenda, wakipata thulúth ya pili, akamwambia, niambie neno la pili.

Akamwambia, mtu akikwambia, umasikini ni bora kuliko utajiri, usimsadiki.