Page:Swahili tales.djvu/412

From Wikisource
Jump to navigation Jump to search
This page has been proofread.

AO RATHI, AO MALI.


Palikuwa na mtu miime na mkewe, wakaomba kwa Muungu kupata kijana, wakapata wa kwanza manamume, na wa pili manamuke. Na baba yao, kazi yake kuchanja kuni. Wakakaa hatta wanakuwa waana wazima. Baba yao akashikwa na ugonjwa. Akawaita waanawe, akawauliza, wataka rathi, ao wataka mali? Yule manamume akamwambia, nataka mali. Manamuke akamwambia, nataka rathi. Akampa rathi babaye sana. Babaye akafa.

Wakakaa matanga, hatta walipoondoka, mama yao akaugua, naye akawaita waanawe, akawaambia, wataka rathi, ao wataka mali? Mwanamume akamwambia, nataka mali. Na mwanamuke akamwambia, nataka rathi. Akampa rathi mamaye yule. Akafa mama yao.

Wakakaa matanga, hatta alipoondoka ikipata siku ya saba. Akaenda mwanamume, akamwambia nduguye mwanamuke, toa vitu vyote vya baba yangu na mama yangu. Akatoa manamuke, asimsazie kitu. Akachukua vyote.

Watu wakamwambia, huyu nduguyo mwanamuke humwachii walao kitu kidogo? Akanena, sitamwachia,