Page:Swahili tales.djvu/402

From Wikisource
Jump to navigation Jump to search
This page has been proofread.
382
PEPO NA MTOTO WA SULTANI.

mbia, chukua. Akaenda nao kwake. Na nyumba kubwa kwake, na killa kitu kimo ndani.

Akawasomesha hatta wakajua elimu pia, wakafanya harufi, akaisha akawapelekea baba yao. Na wale vijana mmoja hodari sana. Akamwambia babao, njoo, tugawanye watoto leo, akamwambia, gawa weye. Akagawanya yee, akatwaa wawili akaweka mbali, akatwaa na mmoja, aka'mweka mbali, akamwambia—Chagua Sultani! Sultani akatwaa wale wawili, na yule akatwaa mmoja, akaenda zake.

Akaenda kwake, akampa funguo zote, akamwambia, killa utakacho fungua. Yule kijana akakaa kitako ndani ya nyumba, na yule babaye kutoka akaenda kutembea mwezi, hatta anaporudi.

Bass, kijana akakaa kitako, hatta siku moja, akachukua ufunguo, akaenda, akafungua chumba kimoja. Akaona thahabu kana maji, akatia kidole ikashika, akaisha kufuta haitoki, akafunga kitambaa. Akaja baba yake, akamwuliza, una nini kidole? Akamwambia, nimejikata. Akakaa hatta siku ya pili, baba yake akatoka, akaenda zake kutembea.

Yule mtoto akachukua funguo zote, akaenda kufungua chumba cha kwanza, akaona mifupa ya mbuzi; akafungua cha pili, akaona mifupa ya kondoo; akafungua cha tatu, akaona ya ngombe, akafungua cha nne, akaona ya punda; akafungua cha tano, akaona ya farasi; akafungua cha sita, akaona vitwa vya watu, akafungua cha saba, akaona farasi mzima.

Akamwambia, ewe binadamu! watoka wapi? Akamwambia, mimi, baba yangu huyu. Akamwambia, kazi yake kula watu, na punda, na farasi, na ngombe, na mbuzi, na killa kitu, na sasa tumesalia mimi nawe.