Page:Swahili tales.djvu/390

From Wikisource
Jump to navigation Jump to search
This page has been proofread.

SUNGURA NA SIMBA.


Aliondoka Sungura kuenda kutafuta chakula mwituni, akaona mbuyu mkubwa sana, akatazama juu, akaona mzinga wa asali ya nyuki. Akarudi mjini kuenda kutafuta wenziwe wa kuja kula naye.

Akapita mlangoni kwa buku, akamkaribisha buku wakakaa kitako. Akamwambia, baba yangu amekufa, ameniachia mzinga moja wa asali, bassi twende tukale. Wakaenda.

Akamwambia, panda juu. Wakapanda wote wawili, wakala asali. Nao wamechukua mienge ya moto, wakachoma nyuki, wakachimbia. Wakazima moto, wakala asali.

Marra akatoka Simba chini ya mbuyu. Akatazama juu, akaona watu wanakula, akawauliza—Nani ninyi? Sungura akamwambia buku, nyamaza, ana wazimo mzee yule. Akawauliza tena, Nani ninyi, hamsemi? Buku akaogopa, akamwambia, sisi hapa.

Sungura akamwambia buku. Nitwae mimi, unitie ndani ya mwenge, umwambie mzee simba, jitenge nitupe mwenge, nami nnakuja. Simba akajitenga, akatupa buku, ukianguka chini sungura akatoka akakimbia.