Page:Swahili tales.djvu/384

From Wikisource
Jump to navigation Jump to search
This page has been proofread.

KISA CHA MWEWE NA KUNGURU.


Aliondoka Sultani ya kunguru, akampelekea waraka Sultani ya mwewe, akamwambia, nataka uwe asikari yangu. Akamwambia sikubali. Akamwambia, kama hukubali tutapigana, mimi nawe. Akamwambia, na tupigane, ukinishinda nitakufuata, nikikushinda weye utanifuata.

Wakapigana, kunguru wakashindwa. Akaondoka mzee mmoja, akawaambia—tukimbie. Wakakimbia katika mji wao, wakaenenda mji mgine. Mwewe walipokuja wasimwone mtu, wakakaa katika mji wa kunguru.

Hatta siku nyingi kunguru wakafanya shauri. Akaondoka mzee, akasema, ninyonyoeni manyoya mkanitupe mjini mwa mwewe. Wakamnyonyoa, wakaenda, wakamtupa.

Walipopita mwewe, wakamwona, wakamwambia, wafanya nini huku mjini kwetu? Akawaambia, wenzangu wamenipiga wamenitoa mji kwa sababu nimewaambia, mfuateni mwewe.

Wale wakamchukua, wakaenda naye kwa Sultani yao, wakamwambia, huyu kunguru tumemwokota, naye mwulize, atasema maneno yake.