Page:Swahili tales.djvu/336

From Wikisource
Jump to navigation Jump to search
This page has been proofread.
316
UZA GHALI.

mali yako hakurudishii, ndio maana, akanena, nimekopesha sitalipwa.

Akamwambia, na'am waziri, inna maneno haya kweli. Sultani akanena, mwenyi kumpa manamke mahari hapati tena, utakapokuwa manamume amefilisika, hafanyi roho yake njema yule manamke kukupa. Kwani umekuwa masikini, akuona kama mjinga, hakujui kama aliokuwa mume wangu, kwani mnekuwa fukara, tena umekuwa mbaya, tena amekufanya mtu mjinga, kwani umekosa mali. Kwani walipokuwa na mali walikuwa manamume mzuri, walikuwa kijana una akili, walionekana kama kijana cha Sultani.

Akaondoka waziri akanena, kweli, Sultani, mtu akikosa mali hawi mtu mbele za watu. Sultani akanena—Waziri, nambie maana ya fungu la nue, kulipa wala hajaisha kulipa.

Akamwambia Sultani, maana yake, Ali alitoa mali katika fungu moja akampa mamaye. Bassi Ali hajui kama mamaye roho yake i rathi kwa mali aliyopewa na mwanawe. Bassi Ali ananena, labuda mama yangu hajafurahi kwa lile nalilomtendea, ndio maana ya kunena Ali, kulipa wala sijaisha kulipa.

Sultani akamwambia, na'am waziri. Akaondoka kitini akasimama, na baraza imejaa tele watu, akamwita akida, akamwambia, nenda gerezani kamwamuru jemadari apige goma, sasa amekuwa Sultani waziri wangu, na mimi ndiye nimekuwa waziri wake; na ninyi jamii asikari, na jamii ya walio mliomo katika mji, Waarabu, na Waswahili, na jamii Wangazidja, mtiini Sultani.

Akiondoka, akautwaa usultani waziri. Bass, wakakaa kitako mda wa siku mbili.