Page:Swahili tales.djvu/328

From Wikisource
Jump to navigation Jump to search
This page has been proofread.
308
UZA GHALI.

Ali akanena, Sultani ameniambia uza ghali si uza rakhisi.

Akaondoka waziri, akamwambia, ntakupa nyumba yangu yote nnaokaa na mali yaliomo yote, illa mke mwana wa watu enda kwao.

Akamwambia, bassi sasa niandikie khati ya mkono wako.

Waziri akamwita Mrashi. Akamwitikia, lebeka, Bwana. Akamwambia, lete kalamu na wino na karatasi kishubakani. Mrashi akaenda akaleta. Waziri akakamata karatasi na wino, akamwandikia Ali, nimempa yote milki yangu kinenacho na kisichonena, hatta nyumba yangu nikaao mwenyewe, illa mke mwana wa watu enda kwao. Akatwaa khati waziri akampa Ali.

Imekuwa saa ya kumi, tuondoke tukasali kwanza, kuregea kwetii kusali nikupe maana zako unazozitaka.

Wakashuka wakaenda zao kusali, wakarudi mosketini. Akawambia, haya, Ali, nambie, kwani tena kumekucha.

Ali akamwambia, maana ya kunena, asiojua maana haambiwi maana, kwa sababu nikimweleza mtu asiokuwa na akili hatajua. Ndio maana killa aniulizaye nikimwambia—asiojua maana haambiwi maana. Na Sultani aliponiita akaniuliza hayaambiwi, kwani Sultani ana akili. Naye, ndiyo akanijibu—Uza ghali, si uza rakhisi. Haya maneno yako.

Bassi nieleze mali haya yalipotea.

Ali akanena, mali haya naliyapiga mafungu manne,