Page:Swahili tales.djvu/326

From Wikisource
Jump to navigation Jump to search
This page has been proofread.
306
UZA GHALI.

itika, lebeka. Kamwambie bibi afanye chakula kwa upesi, kabla saa ya nane hajapiga, na wewe regea.

Alipokuja Mrashi, akamwambia, nimekuja, Bwana. Akamwambia, Mrashi, ukafungue kasha, lete kitambi kimoja cha kilemba, ulete na kofia moja nyeupe ya darizi, lete na kanzu moja ya khuzurungi, ulete na kikoi kimoja seyedia ya uzi, na zote nimefunga pamoja katika bahasha ya leso nyekundu, upesi ulete.

Akaondoka waziri akamwambia Ali, nimekwitia kheri, tafáthali maneno yangu haya asijue mtu, weka ndani nafsi yako. Ali akamwambia, Ee Walla, Bwana, mimi maneno yako nayaweza kuyatoa, Bwana?

Akamwambia, nataka, Ali, unipe maana ya maneno yale waliyomwambia Sultani, unipe na maneno aliokujibu Sultani.

Akamwambia, Sultani ameniambia, Uza ghali, si uza rakhisi.

Ali, Ali, utafáthali ukanambie maneno haya, utanambiaje, na Sultani ameniambia, uza ghali, si uza rakhisi? Ntakupa shamba langu.

Akamwambia, Sultani ameniambia, uza ghali si uza rakhisi.

Akamwambia, Ali, bokhari zangu zote twaa zilio mjini.

Ali akanena, Sultani ameniambia, uza ghali si uza rakhisi.

Waziri akanena, Ali, twaa yote mashamba yangu.

Ali akanena, Sultani ameniambia, uza ghali si uza rakhisi.

Waziri akamwambia, twaa yote milki yangu.

Ali akanena, Sultani ameniambia, uza ghali si uza rakhisi.

Waziri akamwambia, twaa kisemacho na kisichosema katika milki yangu mimi waziri, nami nambie maneno haya.