Page:Swahili tales.djvu/316

From Wikisource
Jump to navigation Jump to search
This page has been proofread.

UZA GHALI, SI UZA RAKHISI.


Aliondoka tajiri mkubwa mwenyi mali mengi, naye waziri wa Sultani. Akakaa katika ulimwengu wake, akazaa kijana kimoja. Na kijana kile, jina lake Ali. Hatta mtoto alipopata mwaka wa khamsi u asherini, babaye akafa. Akasalia yeye na mamaye.

Akarithi mali yake Ali, akatumia mali sana. Hatta Ali akafilisika, akawa maskini thalili pasiwe mtu mmoja amjuaye katika mji ule, rafiki zake yeye, wala wa babaye. Akawa mtu kijana, akatembea katika mji.

Killa amwonaye Ali humwuliza, mali yako waliyatendani, Ali, hatta ukafilisika upesi? Kwani babayo aliacha mali mengi, ungekuwa na akili Ali, mali yako ungedumu nayo. Ali akanena, asiojua maana, haambiwi maana.

Ikawa kazi, neno lake, killa amwulizao humwambia—asiyojua maana, haambiwi maana. Hatta yale maneno mji mzima watu wamejua, kamma Ali, akimwuliza—mali yako umeyatendani, hukujibu, asiyojua maana, haambiwi maana.

Hatta maneno yakafika kwa Sultani. Watu waka-