Page:Swahili tales.djvu/302

From Wikisource
Jump to navigation Jump to search
This page has been proofread.
282
SULTANI MAJINUNI.

u'mue. Bass killa apitaye pale akatoa ada, na yule kijana akakaa na mamaye sana, akakaa na babaye sana.

Baba akapatikana na farathi, akafa, yule mamaye akafanya hathari, nisije nikafa kabla sijamwoza mwanangu. Akamtafutia mwanamke mwanawe, kwa juhudi, mke jamaa yake, mzuri, kijana. Akaoa, akaingia nyumbani, akakaa sana na mkewe, akakaa sana na watu katika mji, na watu wakampenda.

Mamaye akapatikana na farathi, akafa. Akakaa msiba wa mamaye, hatta akatoka, walipokwisha toka msiba, akawaita wale nduguze watatu waanaume; akawaambia, ndugu zangu, nipeni shauri, baba amekufa, na mama amekufa, na hii enzi baba amenipa mimi kabla hajafa.

Wakamwambia baba yetu amekupa enzi, baba yetu kukupa kwako tama, hairudi. Wakamwambia, bassi sasa ndugu yetu wewe, sisi nduguzo tupatie chakula na nguo za kuvaa, hatutaki kitu zayidi, nasi tuko chini yako, lilo utwambialo ndilo tutakalotenda.

Akawaambia, ndugu yangu mkubwa kuwa ndio waziri, na wewe wa kati uwe ndio akida, na wewe wa mwisho ndio karani wangu.

Wakakaa kitako, yeye na nduguze, kwa mashauri mema. Killa mtu akamwoza mke, wakakaa na wake wao, wakakaa na mji wao. Killa mtu akazaa na watoto wao, wakapatana mashauri kama watu wapatanavyo.

Hii ndio hadithi alioifanya Chuma, kumfanyizia Sultani Majnuni, na huu ndio mwisho wa hadithi. Ikiwa njema, njema yetu wote, na ikiwa mbaya, mbaya yangu mimi pekeyangu, nalioifanya.