Page:Swahili tales.djvu/298

From Wikisource
Jump to navigation Jump to search
This page has been proofread.
278
SULTANI MAJINUNI.

Wakaulizana, Je! nyama yule tumempata? Killa mtu akanena, tumempata, bwana. Bassi natulale, hatta ussubui tutazame.

Wakalala hatta ussubui, wakapika wali, wakala, wakanywa maji. Wakaenda, wakazunguka kule nyuma ya mlima. Wakamkuta yule nunda amekufa. Wakashuka hatta wakafika chini, wakamtazama amekufa. Yule mtoto akafurahi sana, na wale watumwa wake wakafurahi. Akawaambia, naona njaa, pikeni tena, tule. Wakatoa mchele, wakapika wali. Wakapika wali mwingi, wakala wali hatta mwingine wakamwaga.

Akawaambia mfungeni, haya, tumkokote. Wakamkokota siku ya kwanza, msitu na nyika, siku ya pili, msitu na nyika, siku ya tatu, msitu na nyika, siku ya nne, nyama tena ananuka. Wale watumwa wake wakamwambia, yule ananuka na tumwache. Akawaambia, huyu tutamkokota hatta utakaposalia mfupa mmoja, tukaende nao kwetu. Hatta alipokoma nuss ya njia, akaimba mtoto,

Mama wee, niulaga
Nunda mla watu. (Marra kumi na mbili.)

Akaenda hatta alipokaribia karibu na mji,

Mwanangu, si yeye
Nunda mla watu. (Marra tano.)

Mama, mama, mama,
Nilawa kumakoikoi, nimbe.
Mama, mama, mama,
Nilawa kumakoikoi, nimbe.
Kumakoikoi, nimbe,
Mama wee, niulaga
Nunda mla watu. (Marra nyingi.)

Mwanangu, ndiyeye
Nunda mla watu. (Marra nyingi hwa kujibiana.)