Page:Swahili tales.djvu/274

From Wikisource
Jump to navigation Jump to search
This page has been proofread.
254
SULTANI MAJINUNI.

wakauawa, wangine wakakimbia. Yule Sultani akarudi na watoto wale, akaja akazika.

Yule mtoto wa saba, alio nyumbani, alipoona khabari zile za nduguzo walipouawa na paka, akamwambia mama, nami nitakwenda, paka aniue kama alivyoua ndugu zangu. Akamwambia, wee utakwendaje mtoto peke yako? Akamwambia, mimi nitakwenda kwa uchungu wa ndugu zangu, siku moja mtu kuondokewa na watu watatu katika dunia, bassi mtu huyu asifanye uchungu? Bassi mimi ntapotea, nikamtafuta yule paka aliowaua ndugu zangu. Akamwambia, vema mwanangu, lakini mimi sipendi uenende. Akamwambia, hawa wamekufa na wende ukafe, juu ya donda si donda? Akamwambia, sina buddi mama ntakwenda kwa jambo hili, wala baba simwambii.

Yule paka tena amekimbia mbali sana. Akafanyizwa mikate na mama yake, akapewa na watu wa kumchukulia vyakula. Akapewa na mkuki mkuu mkali kama wembe, na upanga wake. Akamwambia, mama buriani. Akatoka, akaenda zake.

Hatta alipokoma viungani akaona jibwa kubwa, akampiga, akamfunga, anamkokota. Akaja anakwimba.

Mamá wee, niulága
Nundá mla wátu.

Hatta akafika hatta karibu na mji. Mama yuko juu, akamwona, akamsikia anakwimba,

Mamá wee, niulága
Nundá mla wátu. (Marra 'nne.)

Akamjibu mamake, akamwambia,

Mwanángu, si yéye
Nundá mla watu.