Page:Swahili tales.djvu/230

From Wikisource
Jump to navigation Jump to search
This page has been proofread.
210
SULTANI MAJINUNI.

viwiliwili vyangu vyote vizima, na viwiliwili vyangu vyote vigonjwa.

Gissi gani, bwana, ugonjwa huu?

Akamwambia, sababu ya ugonjwa huu ni sababu ya kuogopa leo baba yangu. Saa ya kwanza ikapiga, ataleta mtu illi kutwaa tende, nami nalimwambia baba yangu, kama kesho saa ya kwanza utalimbuka tende. Bassi mimi tena simekuwa mwongo, mimi simekuwa mpumbavu, nami baba atanifukuza kama amemfukuza ndugu yangu, kwa sababu ya kukosa kula tende.

Akamwambia, bass, bwana, utafanyaje, na jambo limekwisha kuwa?

Ah! bassi nitafanyaje tena? Nitakwenda mimi kabla hajamleta mtu hapa.

Akitoka akaenda zake. Hatta akifika katika njia amkuta mtu akichukua kombe kubwa, na kitambaa cheupe cha kufunikia tende, na kisu kikali cha kukatia tawi la mtende. Akamwambia, Je! unakwenda api? Akamwambia, nimetumwa na babako kuja kwako. Baba yako amenituma kukata tawi moja la mtende lilioiva, unitilie katika kombe hili nipeleke. Akamwambia, Yeye baba ataka zilizoiva, tende hizo mbichi zipo, rudi, twende zetu. Akamwambia, Ee walla.

Hatta alipofika mwangoni pao, akamwona baba yake amekaa kitako, yee na nduguze watu wanne. Akamwambia, Bwana, Sabalkheiri! Akamwambia, karibu. Akamwambia, umemwona mtu naliomleta? Akamwambia, nimemwona, Bwana. Nimemwambia, umkatie tawi la tende laliowiva. Akamwambia, licha laliloiva, hatta bichi liko?

Ah! wamekwenda fanya nini wee? Watu walinena,