Page:Swahili tales.djvu/170

From Wikisource
Jump to navigation Jump to search
This page has been proofread.

HEKAYA YA MOHAMMADI MTEPETEVU.


Yalikuwa zamani za Kalifa, Amiri al Muhminina, Haruni Rashidi, alikaa kitako katika baraza yake, na mawaziri yake. Akamwona kitwana akiingia. Akamwambia, Bibi salaamu, sitti Zubede, baada ya salaam, amefanyiza taji ya kuvaa, amepungukiwa na johari moja, bassi mtazamie johari moja, ilio kubwa. Akatazama katika makasha yake, akatafuta, asipate ilio kubwa kama atakaye.

Akamwambia, niletee ile taji, niitazame. Akamletea taji, imefanywa kwa johari tupu. Akawaambia mawaziri yake, waliokaa naye. Akawaonyesha na taji, akawaambia nataka johari itakayofaa juu ya taji.

Ikawa kulla mtu kutoka kwenda nyumbani kwake kutafuta johari, atakayo kalifa, killa mtu akatafuta asipate. Walizo nazo ndogo, hazifai juu ya taji. Akaingia mjini kwa matajiri, kutafuta johari ilio kubwa, isipatikano.

Mtu mmoja akanena, akamwambia Kalifa, Johari itakayofaa, hapa katika inchi ya Baghdadi haipatikani: