Page:Swahili tales.djvu/136

From Wikisource
Jump to navigation Jump to search
This page has been proofread.
116
SULTANI DARAI.

namke akasituka, akauliza, hawezi nini? Akamwambia, mwili wote, bwana, wamwuma, hana pahali pamoja pasipomwuma.

Ah! bassi, miye nifanyeje, tazama mtama, ule wa felefele, mfanyizia uji, mpe. Yule mkewe akasangaa, amwambia, Bwana, unakwenda kumwambia kufanyiziwa paa uji mtama wa felefele, hatta frasi anaopewa hali aukataa? Eh! Bwana, si mwema wee.

Akamwambia, Oh! ondoka huko, una wazimu wali watu hutupa tu, huko kupata mtama yeye ni haba?

Akamwambia, Kama yule, bwana, si paa, ni mboni yakwe ya jicho, likiingia mchanga, utaingia na shughuli.

Ah! maneno yako mengi, mwanamke saa!

Akaenda yule mzee hatta chini. Yule mzee alipomwona paa, akasangaa, akitoka na machozi sana, akalia sana. Ah! paa!

Akamwuliza, gissi gani, mama? Nimekutuma na kurudi na kulia tu, hunijibu naliokutuma? Likiwa jema, nijibu, na likiwa baya, nijibu, kwani hii ndio hali ya ulimwengu wakimtenda vema mtu atakutenda mabaya. Bassi sikutendwa mimi tu, wametangulia na watu zamani wakatendwa kama haya. Akamwambia, bassi nambie.

Akamwambia, kinwa kimejaa mate, na ulimi wangu umejaa kinwani, siwezi kukwambia kama hayo nalioambiwa, wala siwezi kukutendea kama haya nalioagizwa.

Akamwambia, Mama wewe waliloagizwa na waliloambiwa kunitendea, nitendee, na uliloagizwa kunambia, nambie. Wala usiogope kwambia, wala si tahayari kuniambia, kwani haya hukuniambia wewe, alionambia mwenyewe namjua, nieleze mama.