Page:Swahili tales.djvu/108

From Wikisource
Jump to navigation Jump to search
This page has been proofread.
88
SULTANI DARAI.

siku saba nirudi, kama sikurudi muda wa siku saba, hatatoka ndani illa nije. Akamwambia, vema, kua heri.

Sultani akamwambia, hutaki watu wakufuate. Akamwambia, mimi nalitumwa kwetu na wingi wa mali, nikaingia katika nyika na katika nyika hamna jambo jema, killa jambo baya asili yake yatoka na nyikani, nami nalikuja hapa pekeyangu nisiogope, sembuse leo nisipochukua kitu nitaogopa mimi? Kua heri bwana, naenda zangu.

Akaenda—a—a katika msitu na nyika hatta akawasili katika mji. Mji ule mkubwa, una majumba mazuri. Akaona ule mji umejiinama, akasangaa, asiweze kwenda, wala asiweze kurudi, akanama, akafikiri, akawaza, akatazama, hakutanabahi jawabu, illa kuingia katika mji. Akaingia. Akafuata njia mkubwa, hatta mwisho wa njia kubwa, kuna nyumba kuu, nyumba mzuri mno isiyokuwa na kifani katika ule mji. Akaiona nyumba umejengwa kwa yakuti, kwa fieruzi, kwa mawe mazuri ya mármár.

Paa akasangaa, akawaza, akafikiri, alipotanabahi, akanena, hii ndio nyumba kwa bwana wangu. Nami nitapiga moyo konde, nende niwatazame watu walio katika nyumba hii, ina mtu ao haina mtu. Kwani nimeanza kuingia katika mji, tokea mwanzo wa mji hatta nimefika hapa kati ya mji, sikupata kumwona mtu awe yote katika mji huu, sikumwona mume, wala mke, wala mzee, wala kijana, hatta nimewasili hapa. Bassi na nyumba hii ntapiga moyo konde niingie. Akanena, kama kufa nitakufa, kama kupona nitapona, kwani mimi hapa sasa nilipo sina hila kwani nitokako mbali, bassi kama kitakachojaliwa kuniua na kiniue.